WAJUMBE WA BODI MPYA YA MAJAI SAFI NA USAFI WA MAZINDIA MJINI NJOMBE ILIVYOKABIDHIWA ZANA ZA KAZI
Hafla ya uzinduzi huo ...imefanyika September 17,2026 katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe na kudhuriwa na watumishi wote wa mamlaka hiyo na wadau kutoka taasisi mbalimbali za kiserikali na kijamii.
Akiwasilisha risala yake mbele ya Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingiri Mjini Njombe (NJUWASA) Mhandisi Robert Lupoja amemshukuru waziri wa Maji Jumaa Aweso kwa kuteua Body mpya baada ya bodi iliyokuwepo kumaliza muda wake June 30 2026.
Amesema Body za mamlaka ya maji nchini huteuliwa na waziri mwenye dhamana na hudumu kwa miaka mitatu na kuteuliwa body nyingine, amesema Mamlaka inawajibu wakuhakikisha jamii inapata huduma bora ya maji safi na salama hivyo uwepo wa bodi hiyo ni chachu katika kuisadia serikali kuhtimiza malengo yake.
Imeelezwa kwamba Njuwasa inahudumia Kata tatu za Mji wa Njombe inatoa huduma kwa wakazi wapatao 97000 ikiwa na uhitaji wa lita za maji zipatazo milioni kumi na laki nne kwa siku lakini inazalisha milioni nne hadi lita milioni tano kwa siku hivyo kuna upungufu.
Mhandisi Lukoja amesema kwa sasa maunganisho ya maji yamewafikia wateja elf kumi na kwa sasa watu wanaopata huduma ya maji safi na salama ni elf sabini na saba na kwa sasa wanashughulikia changamoto hizo kwa kutetekeleza mradi wa maji wa chanzo cha Lugenge unaozalisha lita milioni 1 kwa siku mradi uko asilimia 100 na uko katika uangalizi.
Lakini pia wanatekeleza chanzo cha Hagafimilo ambao ni mradi wa miji 28 ambao utaongeza lita milioni 11 kwa siku na uko asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika mwezi November 2026 na pia wanatekeleza mradi wa upandaji miti ili kuhifadhi vyanzo vya maji.
Watumishi wa Njuwasa kwa sasa wanafanya kazi hadi siku za mapumziki na sasa wamekwisha kutumia mfumo wa malipo ya kabla katika huduma za zamaji hatua ambayo itaiwezesha mamlaka kukusanya mapato kwa wakati na kutatua changamoto zingine.
Eunis Vuhahula Lwendo ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi aliyemaliza muda wake muda wake ameeleza mafanikio waliyoyapata wakati wa uongozi wao kuwa ni pamoja na kufanikiwa kuongeza idadi ya watumishi 46 waliokuwepo mwaka 2023 na kufikia watumishi 60 kwa mwaka 2026 wakati bodi inamaliza muda wake.
Aidha bodi hiyo iliyomaliza muda wake imefanikiwa kusomesha watumishi 15 na watumishi 5 walihitimu mafunzo yao katika fani mbalimbali na kwa kipindi chote hicho hakukuwa na mashauri ya jinai na nidhamu au malalamiko ya watumishi na wamefanikiwa kusimamia miradi miradi 8 inayoenelea na utekelezaji wake kwa sasa kwa weledi mkubwa.
Ndg, Fidelis Lumato ni Mwenyekiti wa Bodi Mpya iliyozinduliwa nae kwa upande wake Ameshukuru kukabidhiwa Taaissi hiyo muhimu na ameahidi kwenda kuhakikisha wanasimamia utoaji wa bora amemshukuru Rais Dr Samia Suluhu Hassani utoa wa fedha za utekelezaji wa miradi, Waziri wa Maji Jumaa Aweso kwa kuwateua na Mkuu wa Mkoa Antony Mtaka kwa kuwaamini na kwa ushirikiano ambao amekua akiwapatia.
Ameahidi kwa kadiri ya uwezo wao watasimamia na kuongoza vyema mamlaka kutekeleza majuku ya kutoa huduma za maji na usafi wa mzingira na watatoa ushirkiano kwa viongozi wote.
Zakaria Mwansasu ndiye aliyekuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo wa Bodi Mpya akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa Antony Mtaka aishukuru Bodi iliyomaliza muda wake na ametoa wito kwa Bodi mpya kwenda kuwatumikia wananchi.
Amewataka wakumbuke wanajukumu kubwa la kuhakikisha Mamlaka ya Maji inakwenda kusimamia na kuwa mfano wa kuigwa katika kutoa huduma bora na uongozi uliotukuka ili wananchi wapate haki ya msingi ya kupaata huduma bora ya maji na amewataka watambue kuwa wanawajibu wakuhakikishwa wananchi wanapata maji kwa utarataibu na wajue wanayohaki ya kulipia hayo maji. See lessShow More



















